7. Asili ya Mwanadamu
Mwanamume na Mwanamke walifanywa kwa mfano wa Mungu wakiwa kila mmoja na nafsi yake, uwezo na uhuru wa kufikiri na kutenda. Ingawa waliumbwa viumbe huru, kila mmoja ni umoja wa nafsi isiyogawanyika ya mwili, akili na roho, akimtegemea Mungu kwa uhai na pumzi na mengine yote. Wakati wazazi wetu wa kwanza walipomwasi Mungu, walikana utegemezi wao kwa Mungu na wakaanguka kutoka hadhi yao ya juu chini ya Mungu. Sura ya Mungu iliyokuwa ndani yao iliharibiwa na wakawa chini ya mauti. Wanazaliwa wakiwa na udhaifu na mivuto ya kuelekea kwenye uovu. Lakini Mungu katika Kristo alipatanisha ulimwengu na nafsi yake, na kwa njia ya Roho wake hurjesha ndani ya wnadamu watubuo sura ya Muumba wao. Wakiwa wameumbwa kwa ajili ya utukutu wa Mungu , wanaitwa kumpenda na kupendana wao wa wao, na kutunza mazingira yao
Mafungu ya Biblia
Mwa. 1:26 – 28; 2:7; Zab. 8:4 – 8; Mtdo. 17:24 – 28; Mwa. 3; Zab. 51:5; Warumi 5:12 – 17; IIWakor. 5:19, 20; Zab. 51:10; IYoh. 4:7, 8, 11, 20; Mwa. 2:15
